WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Thursday 17 September 2015

UJUMBE WA KAMPUNI YA POLY TECHNOLOGIES, INC. YA CHINA WAMTEMBELEA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI , MHE. MATHIAS CHIKAWE OFISINI KWAKE

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akimkaribisha Makamu wa Rais wa Kampuni ya Poly Technologies, Inc. ya China Bw. Huang Geming (mwenye tai) aliyeongoza ujumbe wa Kampuni yake kumtembelea Waziri ofisini kwake.

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (katikati) akiongea na ujumbe wa Kampuni ya Poly Technologies, Inc. ya China (haupo pichani) uliomtembelea ofisini kwake. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil na na kulia ni Katibu wa Waziri, Nelson Kaminyoge.

 Ujumbe wa Kampuni ya Poly Technologies, Inc. ya China, ukiongozwa na Makamu wa Rais wa Kampuni hiyo Bw. Huang Geming (wa tatu toka kulia) katika mazungumzo ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi (hayupo pichani) ulipomtembelea Waziri huyo ofisini kwake.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (katikati) katika picha ya pamoja na ujumbe wa Kampuni ya Poly Technologies, Inc. ya China uliomtembelea ofisini kwake.  Wa pili kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil.

No comments:

Post a Comment