WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Thursday 3 July 2014

KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA JOHN MINJA AKABIDHI ZAWADI KWA WAFANYAKAZI BORA RAIA WA JESHI HILO JIJINI, DAR ES SALAAM

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(kushoto) akikabidhi cheti kwa Mfanyakazi bora kwa Mwaka 2014, Bw. John Chacha(kulia) ambaye ni Mhudumu wa Ofisi daraja la pili katika Ofisi ya Magereza Mkoani Mwanza. Zawadi kwa Wafanyakazi raia wa Jeshi la Magereza hutolewa kutokana na utendaji mzuri wa kazi pamoja na nidhamu kazini. Hafla hiyo ya kukabidhi zawadi kwa Watumishi hao imefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi Bora wa Jeshi la Magereza kwa Mwaka 2014 ambao wamekabidhiwa zawadi zao leo na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(hayupo pichani) wakisikiliza  kwa makini wakati Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Jeshi la Magereza alipokuwa akitoa neno la shukrani kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza katika hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Wafanyakazi Bora wa Jeshi la Magereza, leo Julai 3, 2014 Jijini Dar es Salaam(katikati) ni Mhudumu wa Ofisi daraja la Pili, Bw. John Chacha kutoka Ofisi ya Magereza Mkoani Mwanza.
 Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza waliohudhuria hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Wafanyakazi bora wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani) wakifurahia jambo wakati Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Jeshi la Magereza alipokuwa akitoa neno fupi la shukrani kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza. Kulia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga(kushoto) ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Clement Keenja.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa nasaha zake fupi katika hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Wafanyakazi Bora raia wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani) kwa Mwaka 2014. Hafla hiyo fupi imefanyika leo Julai 3, 2014 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Jeshi la Magereza, Bw. Sedumba Katenda(katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza mara tu baada ya hafla fupi ya kukabidhiwa zawadi kwa Wafanyakazi bora wa Jeshi la Magereza. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 3, 2014 katika Ofisi ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment