WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Thursday 26 June 2014

KIKAO CHA ISHIRINI NA SITA CHA BODI YA TAIFA YA PAROLE CHAFANYIKA MWANZA HOTELI, JIJINI MWANZA

Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Jaji Mstaafu Eusebia Munuo (kushoto) akiongoza kikao cha kujadili Wafungwa waliopendekezwa kuachiliwa kwa Parole. Kulia ni Kaimu Katibu wa Bodi ya Taifa ya Parole, Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa. Kikao hicho cha siku mbili kimeanza leo Juni 26, 2014 katika Ukumbi wa Mwanza Hoteli, Jijini Mwanza.


Baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Taifa ya Parole wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole Jaji Mstaafu Eusebia Munuo (hayupo pichani) wakati akitoa hoja ya kufungua Kikao cha kupitia mapendekezo ya Wafungwa waliopendekezwa kuachiliwa kwa Parole (wa kwanza kulia) ni Francis Stolla akiwa na Wajumbe wenzake wakipitia makabrasha ya mapendekezo hayo.


Wajumbe wa Sekretarieti ya Taifa ya Parole wakifuatilia majadiliano katika Kikao cha Bodi ya Taifa ya Parole (wa kwanza kulia) ni Afisa Mwandamizi Kitengo cha Parole, Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Rose Odemba wakifuatilia kwa makini majadiliano ya Wafungwa watakaoachiliwa kwa Parole (katikati) ni Mjumbe wa Sekretarieti ya Bodi ya Taifa ya Parole, Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Bruno Pancras (wa kwanza kushoto) ni Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Merikior Komba.

Wajumbe wa Bodi ya Taifa ya Parole wakiwasili katika Ukumbi wa Mwanza Hoteli tayari kwa Kikao cha Bodi ya Taifa ya Parole kitakachofanyika kwa siku mbili kuanzia leo Juni 26, 2014 katika Ukumbi wa Mwanza Hoteli, Jijini Mwanza (wa kwanza mbele) ni Mjumbe wa Bodi, Ayub Mwenda toka Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Nchini(kushoto) ni Jonas Tarimo, Mjumbe wa Bodi ya Taifa ya Parole toka Ofisi ya Kamishna wa Ustawi wa Jamii.


Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Mhe. Jaji Mstaafu Eusebia Mnuo (kushoto) akifanya mahojiano Maalum na Waandishi wa Habari kabla ya kuanza rasmi kwa Kikao cha Ishirini na Sita cha Bodi ya Taifa ya Parole mapema leo Juni 26, 2014. Kikao hicho kitafanyika kwa siku mbili katika Ukumbi wa Mwanza Hoteli, Jijini Mwanza. (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment