WAZIRI wa Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe amekutana na
Mwanaharakati wa Kimataifa wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel
na kujadili masuala mbalimbali ya haki za wanawake na watoto katika Hoteli ya
Serena jijini Dar es Salaam leo.
Katika mazungumzo yao,
Waziri Chikawe alimwambia mke huyo wa Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson
Mandela, juhudi zake za kuingiza katika
Katiba Mpya kifungu cha kuzuia mtoto wa chini ya miaka 18 asioe wala asiolewe.
Hata hivyo, Mama Machel
kwa upande wake alimshukuru Waziri Chikawe kwa maoni yake na kusema kuwa ni
muhimu kwa wadau wote wa haki za watoto wakashinikiza wajumbe wa Bunge Maalum la
Katiba na watunga sheria wote wahakikishe kipengele hicho kinaingia ndani ya
Katiba. Mama Machel yupo nchini kuhudhuria mkutano wa ufunguzi wa Kampeni ya
Kitaifa ya kutokomeza ndoa za utotoni.
No comments:
Post a Comment