JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI
LA POLISI TANZANIA
PRESS RELEASE
02/09/2014
ANAYEJIFANYA AFISA USALAMA WA TAIFA ANASWA
DAR ES SALAAM
Mtu mmoja
anashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam kutokana na makosa
mbalimbali ya kujifanya ni mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa. Mtu huyo
anayejulikana kwa jina la GUNNER S/O SAIMON MEENA, Miaka 40, Mkazi wa Kinyerezi
Segerea anatuhumiwa kuwasumbua wafanyabiashara mbalimbali jijini Dar es Salaam
kwa kuwasingizia au kuwatuhumu kwamba wanahusika na makosa yenye kuhatarisha
usalama.
Kwa muda mrefu Jeshi
la Polisi limekuwa likimtafuta mtu huyo kutokana na malalamiko mengi ambayo
yamekuwa yakijitokeza na uchunguzi unaonyesha kwamba jina lake halipo katika
orodha ya watumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa.
Tukio la mwisho
lililomfanya akamatwe ni pale alipomtishia mfanyabiashara mwenye asili ya
kisomali aitwaye ABDI S/O MOHAMED
DALMAR. Katika tishio hilo la kutishia mtuhumiwa GUNNER S/O SAIMON MEENA ambaye
ni Afisa Usalama feki alidai apatiwe kiasi cha fedha za kitanzania TSHS 25,000,000/= (SHILINGI MILLIONI ISHIRINI NA TANO) ama sivyo angechukuliwa hatua
chini ya sheria ya Usalama wa Taifa.
Mlalamikaji alitoa
taarifa na ndipo mtuhumiwa akakamatwa
katika mtego wa Polsi. Uchunguzi zaidi wa shauri hili unafanyika na mtuhumiwa
atafikishwa mahakamani baada ya jalada la kesi yake kupitiwa na mwanasheria wa
Serikali.
S. H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM
No comments:
Post a Comment