WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Monday 30 March 2015

WAZIRI CHIKAWE AONGOZA MATEMBEZI YA HISANI KUPINGA MAUAJI YA ALBINO

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (aliyevaa jaketi lenye ramani ya Tanzania) akiwa na mamia ya washariki wa matembezi ya hisani ya kuhamasisha kukomeshwa kwa mauaji ya watu wenye ualbino nchini. Matembezi hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Imetosha yalianza katika viwanja vya Biafra na kuishia viwanja vya Leaders Club wilayani Kinondoni, ambapo vikundi mbalimbali vya mazoezi ya viungo jijini Dar es Salaam vilishirikishwa pamoja na wageni waalikwa akiwemo Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaimar Kweigyir (kushoto kwa Waziri) pamoja na Jaji wa Mahakama Kuu, Hamisa Kalombola (kulia kwa Waziri).
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wanne kulia), Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaimar Kweigyir (wanne kushoto), Jaji wa Mahakama Kuu, Hamisa Kalombola (watatu kushoto) pamoja na Viongozi na Wanaharakati wa Taasisi ya Imetosha inayopambana na kutokomeza mauaji ya watu wenye ualbino nchini wakiimba wimbo wa Tanzania Nakupenda katika viwanja vya Leaders Club mara baada ya kufanya Matembezi ya Hisani yaliyoanzia viwanja vya Biafra Kinondoni jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo yaliandaliwa na Taasisi hiyo kwa kuwashirikisha mamia ya washariki kutoka katika vikundi mbalimbali vya mazoezi ya viungo jijini Dar es Salaam pamoja na wageni waalikwa.
Mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akitoa hotuba yake yenye kulaani mauaji ya albino nchini mbele ya viongozi na wanaharakati wa Taasisi ya Imetosha inayopambana na kutokomeza mauaji ya watu wenye ualbino nchini pamoja na mamia ya washiriki wa Matembezi ya Hisani (hawapo pichani). Katika hotuba yake, Chikawe aliwaomba wananchi washirikiane na serikali kikamilifu katika kuwalinda watu wenye ualbino ili kusambaratisha mauaji hayo ambayo yanaendelea hasa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa. Hata hivyo, Chikawe alisema Jeshi la Polisi linaendelea kuwakamata watuhumiwa pamoja na kutoa ulinzi mkali kwa albino, pia alisema Serikali itashirikiana na Taasisi hiyo ili kuendelea kupinga ukatili huo wanaotendewa albino. Waziri Chikawe alisema hayo baada ya kushiriki matembezi hayo yaliyoanzia viwanja vya Biafra na kuishia viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam leo.

 Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaimar Kweigyir (watatu kushoto), washiriki wa Matembezi ya Hisani ya kupinga mauaji ya albino wakishangilia mara baada ya kufanya matembezi hayo yaliyoandaliwa na Viongozi na Wanaharakati wa Taasisi ya Imetosha inayopambana na kutokomeza mauaji ya watu wenye ualbino nchini. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (hayupo pichani), aliyaongoza matembezi hayo yaliyoanzia viwanja vya Biafra na kuishia viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam leo na kuwaomba wananchi washirikiane na Serikali kuwalinda watu wenye ualbino ili kusambaratisha mauaji hayo ambayo yanaendelea nchini.
Balozi wa Taasisi ya Imetosha ambaye pia ndiye mwanzilishi wa Taasisi hiyo, Henry Mdimu akitoa hotuba yake fupi kwa mgeni rasmi pamoja na mamia ya washiriki (hawapo pichani) wa matembezi ya hisani ambayo yaliandaliwa na taasisi hiyo ikiwa ni Kampeni Maalum ya kupinga mauaji ya albino nchini. Kwa mujibu wa Mdimu, taasisi yake inatarajia kwenda katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ili kutoa elimu kwa wananchi hao kuhusiana na imani potofu dhidi ya mauaji ya albino.
Sehemu ya washiriki wa Matembezi ya Hisani ya kupinga mauaji ya albino nchini wakifanya mazoezi ya viungo baada ya kufanya matembezi hayo yaliyoandaliwa na Viongozi na Wanaharakati wa Taasisi ya Imetosha inayopambana na kutokomeza mauaji ya watu wenye ualbino nchini. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (hayupo pichani), aliyaongoza matembezi hayo yaliyoanzia viwanja vya Biafra na kuishia viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam na kuwaomba wananchi washirikiane na Serikali kuwalinda watu wenye ualbino ili kusambaratisha mauaji hayo ambayo yanaendelea nchini.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Imetosha, Masoud Kipanya (kulia) akielezea jinsi yeye pamoja na Balozi wa Taasisi hiyo, Henry Mdimu (kushoto) pamoja na viongozi wengine wa taasisi hiyo, walivyopania kuhakikisha wanasambaratisha mauaji ya albino nchini. Taasisi hiyo imefanya matembezi ya hisani ikiwa ni kampeni maalum ya kupinga mauaji ya albino nchini. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (hayupo pichani), aliyaongoza matembezi hayo yaliyoanzia viwanja vya Biafra na kuishia viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam na kuwaomba wananchi washirikiane na Serikali kuwalinda watu wenye ualbino ili kusambaratisha mauaji hayo ambayo yanaendelea nchini

No comments:

Post a Comment