WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Wednesday 25 March 2015

MPANGO WA ULINZI JIRANI

JINSI YA KUTAMBUA VITENDO VYENYE KULETA SHAKA YA UHALIFU


·        Ni muhimu kuwa macho wakati wowote kwa jambo lolote linalotendeka nje ya utaratibu. Kwa mfano, tendo linafanyika muda ambao sio wa kawaida kama vile usiku au mahali ambapo sio pa kawaida kwenye kificho.  Tendo kama hilo linaweza kuashiria uhalifu.
·        Kuwepo kwa mtu au watu wasio wakazi wa eneo, wanaopitapita mtaani bila sababu maalumu.


·        Kuwepo kwa milango au madirisha yaliyo wazi au kuvunjwa katika eneo ambapo daima huwa limefungwa au nyumba ambayo haina watu. Hii inaweza kuwa ashirio la tendo la uvunjaji wa nyumba.
·        Kuwepo kwa karakana za kificho kunaweza kuashiria ni mahali maalumu pa kubadili alama, namba au umbile la chombo kilichoibiwa.
·        Kusikia sauti au kelele ambazo sio za kawaida kama vile mlio wa bunduki, kupiga yowe, au mbwa kubweka kwa muda mrefu.  Hili linaweza kuwa ashirio la kutendeka tendo la uhalifu.


·        Mtu kuonyesha ishara za kiakili au kimwili ambazo sio za kawaida.  Inawezekana mtu akawa ameumizwa, ana athari za madawa ya kulevya au anahitji msaada wa matibabu.

VITENDO KAMA HIVI VINAPOONEKANA KATIKA ENEO LAKO WAJULISHE  MAJIRANI NA TOA TAARIFA KATIKA SERIKALI YA MTAA AU POLISI KWA KUTUMIA SIMU YA DHARURA.


No comments:

Post a Comment