WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Monday 23 March 2015

USALAMA WETU

JUKUMU LA WANANCHI KATIKA MPANGO WA ULINZI JIRANI

Majukumu ya Msingi ya Wananchi katika Mpango wa Ulinzi Jirani:

·         Kuwa macho na masikio ya masuala ya ulinzi na usalama katika eneo lao.

·         Wananchi wana jukumu la kushirikiana na Polisi katika kutafuta ufumbuzi endelevu wa matatizo ya kiusalama yanayojitokeza ndani ya jamii yao.

·         Kwa pamoja watapanga mipango inayotekelezeka ya kujihakikishia usalama wa maisha na mali.

·         Ulinzi jirani ni moja ya mipango inayotekelezeka kirahisi na bila gharama.

Kama mpango wa Ulinzi Jirani utapangwa vema na kutekelezwa kwa ushirikiano mzuri wa wananchi na Jeshi la Polisi, mambo makuu yatajitokeza katika jamii:

·         Makazi ya wananchi yatakuwa salama na yenye amani na utulivu kwa kuwa wahalifu watatokomea.

·         Ushirikiano baina ya wananchi na Jeshi la Polisi utakuwa wa karibu na utaimarika hivyo uhalifu utadhibitiwa.











No comments:

Post a Comment