WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Monday 8 February 2016

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YAANZA KAZI RASMI - YAPOKEA TAARIFA YA UTENDAJI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akijitambulisha kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kabla ya Kamati hiyo kuipokea taarifa ya Wizara hiyo katika kikao cha kwanza cha Kamati hiyo baada ya kuundwa na Bunge hivi karibuni. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu anayefuatia ni Makamu wake, Kanali Masoud Khamis. Kulia kwa Masauni ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Mohamed Rajabu akizungumza jambo na Wajumbe wa Kamati yake pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika kikao chao kwanza tangu Kamati hiyo iundwe na Bunge hivi karibuni.  Wapili kulia mstari wa mbele ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni, na kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Kanali Masoud Khamis. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akitoa taarifa ya Wizara katika kikao cha kwanza cha Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kikao hicho kilichohudhuriwa na Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na Maafisa wa Wizara, kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama  na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Injinia Hamad Masauni (hayupo pichani) alipokuwa anawasilisha taarifa ya Wizara kwa Kamati hiyo katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni (katikati) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira wakiiweka sawa taarifa ya wizara yao kabla ya kuiwasilisha kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu. Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na Watendaji wa Wizara walikutana katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo, kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya Ulinzi na Usalama. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
 

No comments:

Post a Comment