WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Saturday 20 February 2016

KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI AFUNGA MKUTANO WA MWAKA WA MAAFISA WAANDAMIZI JESHI LA POLISI NCHINI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kulia), akipokelewa na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Ilala, SACP Lucas Mkondya, alipofika kufunga kikao  kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, akizungumza wakati wa kufunga kikao  kazi cha Maafisa Maandamizi wa Jeshi la Polisi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Wapili kulia meza kuu ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, akizungumza na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi nchini wakati wa kufungwa Mkutano wa Mwaka wa Maafisa hao uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu (kulia), akimpongeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, mara baada ya Katibu Mkuu huyo kumaliza kutoa hotuba ya kufunga Mkutano wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (wanne kushoto waliokaa), Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu (kushoto kwa Katibu Mkuu) wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi, mara baada ya kufungwa Mkutano wao wa Mwaka uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment