WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Sunday 18 May 2014

WAZIRI CHIKAWE AUNGANA NA MAAFISAWAKE KUSHANGILIA KUPITISHWA BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI, BUNGENI DODOMA

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akipokea pongezi kutoka kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu, Mwamini Malemi (katikati) mara baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuipitisha Bajeti ya Wizara hiyo katika Bunge la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Haji Janabi (kushoto) akimpongeza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (kulia) kwa kuyajibu kwa ufasaha baadhi ya maswali ya Waheshimiwa Wabunge na hatimaye Bajeti ya wizara hiyo ya Mwaka wa Fedha 2014/15 kupita. Kulia kwa Naibu Waziri Silima ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil na Naibu Katibu Mkuu, Mwamini Malemi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wapili kulia) akimfafanulia Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, jinsi alivyoyajibu maswali ya waheshimiwa wabunge kabla ya kupitishwa Bajeti ya wizara hiyo ya Mwaka wa Fedha 2014/15. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) wakipongezana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Pereira Ame Silima kwa kuyajibu maswali mbalimbali ya waheshimiwa wabunge na hatimaye Bajeti ya wizara yao kupitishwa na Bunge la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma. Nyuma yao, Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil na Naibu Katibu Mkuu, Mwamini Malemi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

No comments:

Post a Comment