WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Friday 20 June 2014

MAADHIMISHO YA SIKU YA MAGEREZA YAFANA JIJINI DAR ES SALAAM


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akipokea Salaam ya heshima toka kwa Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maafisa wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani) katika maadhimisho ya Siku ya Magereza(Magereza Day). Kushoto katika picha ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja (kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Maafisa wa Magereza Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Erasmus Kundy.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akikagua Gadi ya Wanawake inayoundwa na Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Magereza Day yaliyofanyika leo Juni 20, 2014 katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa wa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam.

Msanii Nguza Viking anayetumikia Kifungo chake Gerezani akiwa na Bendi ya Wafungwa(anayepiga gitaa) akiimba Wimbo Maalum kuhusu Urekebishaji wa Wafungwa unavyofanyika Magerezani(wa pili kulia) ni Jonson Nguza Maarufu kwa jina la Papii Kocha wakitumbuiza katika Maadhimisho ya Magereza Day yaliyofanyika leo Juni 20, 2014 katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(aliyesimama) akitoa maelezo mafupi kuhusu Madhumuni ya Maadhimisho ya Siku ya Magereza(Magereza Day). Maadhimisho haya ya siku ya Magereza yanafanyika hapa nchini kwa mara ya pili ambapo leo yamefanyika katika Chuo cha Maafisa wa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam(wanne kulia katika vazi la suti nyeusi) ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe, (wa pili kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Namibia, Raphael Tuhaferi.

Mkuu wa Kitengo cha Kilimo na Mifugo Ndani ya Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mlasan Kimaro (wa pili kushoto) akitoa maelezo mafupi kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (suti nyeusi) kuhusu uzalishaji wa mafuta ya mawese ambayo hutumika kwa matumizi ya Wafungwa Magerezani alipotembelea Banda la Kilimo na Mifugo. Wapili kulia kwa Waziri ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja.

No comments:

Post a Comment