WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Monday 16 June 2014

[wanabidii] UHAMIAJI WAMEONYESHA UWAZI KATIKA USAILI



Saturday, June 14, 2014 0
Ndugu zangu ,

Toka juzi nimeona watu kadhaa wakiponda hatua ya Idara ya uhamiaji kuita kwenye usaili watu zaidi ya alfu 1 wakati wanaotakiwa ni watu 70 tu .

Kuna jamaa wamechukulia hili kama ajenda ya kisiasa na kuanza kuhoji au kurushia vijembe vyama vingine vya kisiasa kusuatia kadhia hiyo .

Tunachopaswa kujua ni kwamba idara ya Uhamiaji ni Nyeti kama zilivyo idara nyingine za kiulinzi na usalama nchini , mchujo wake unahusisha vitu vingi sana kuliko ilivyo awali , sio elimu tu na afya tu kuna masuala ya uelewa wa vitu mbalimbali , historia yako ya nyuma , mahusiano yako na hata kwenye mafunzo na mazoezi kabla ya kuanza kazi rasmi .

Kwahiyo ukichukuwa watu hao alfu 1 au 2 , ukiwaweka kwenye mizani hiyo unaweza kupata hao 70 au usipate kabisa kutegemeana na vigezo vilivyowekwa na idara yenyewe .

Naipongeza idara kwa hatua yake ya kuwa wazi kwa kuita watu kwa mkupuo sehemu moja kwa ajili ya usaili , maana pale msailiwa anaangaliwa toka wakati anaingia uwanjani , atakavyowasiliana na wenzake na masuala mengine mengi , ndio tupo kwenye dunia hiyo ya kuangaliana kabla ya majukumu .

Tumeona operesheni ya kuondoa wahamiaji haramu ilivyoleta madudu mengi nchini mpaka kuundwa kamati na wengine kujiuzuru , hatupendi hiyo itokee tena ndio maana usaili unatakiwa uwe wa makini , wawazi na wenye viwango .

Tusipende kuponda na kudharau kila kitu haswa hivi vinavyohusu usalama wetu wenyewe .
...........................
Yona Fares Maro

No comments:

Post a Comment