WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Saturday 19 July 2014

WAZIRI CHIKAWE AFUTURISHA WATOTO YATIMA JIMBONI KWAKE NACHINGWEA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe, akifurahi na Watoto Yatima na Waishio katika Mazingira Hatarishi wa Kituo cha Nawoda mjini Nachingwea mkoani Lindi kabla ya kufuturu nao futari maalum aliyoiandaa kwa ajili ya watoto hao zaidi ya 80 ambao wanalelewa katika kituo hicho. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto), akijiandaa kufuturu na Watoto Yatima na Waishio katika Mazingira Hatarishi wa Kituo cha Nawoda mjini Nachingwea mkoani Lindi. Waziri Chikawe aliandaa futari maalum kwa ajili ya watoto hao zaidi ya 80 ambao wanalelewa katika kituo hicho.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (katikati), akizungumza jambo na Shekhe Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Abdul Mpakate (watatu kulia) wakati wa kufuturu futari maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya Watoto Yatima na Waishio katika Mazingira Hatarishi wa Kituo cha Nawoda mjini Nachingwea mkoani Lindi. Waziri Chikawe aliandaa futari hiyo kwa watoto zaidi ya 80 wanaolelewa katika kituo hicho.

Shekhe Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Abdul Mpakate akitoa dua la kumshukuru Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto), kwa kuandaa futari maalum kwa ajili ya Watoto Yatima na Waishio katika Mazingira Hatarishi wa Kituo cha Nawoda mjini Nachingwea mkoani Lindi. Waziri Chikawe aliandaa futari hiyo kwa watoto zaidi ya 80 wanaolelewa katika kituo hicho. Picha zote na Felix Mwagara.

No comments:

Post a Comment