WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Monday 4 August 2014

MAASKOFU MORAVIAN WATINGA OFISINI KWA CHIKAWE, WAMUOMBA AINGILIE KATI MGOGORO NDANI YA KANISA



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akimsikiliza kwa makini Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian nchini, Alinikisa Cheyo (wapili kushoto) wakati wa mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi ya Waziri Chikawe jijini Dar es Salaam leo. Maaskofu watano wa Kanisa hilo ambalo limekumbwa na mgogoro kwa muda mrefu sasa walionana na Waziri huyo ili kuomba msaada wake katika kudhibiti vurugu zinazoendelea katika Kanisa hilo. Hata hivyo, Waziri Chikawe aliahidi kulifanyia kazi na hatimaye kulitolea maamuzi suala hilo baada ya kufanya uchunguzi wa kina kwa kukutana na pande zote mbili zinazogombana. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akizungumza na Maaskofu wa  Kanisa la Moravian nchini baada ya kuwasikiliza malalamiko yao kuhusiana na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea kwa muda mrefu katika Kanisa hilo. Maaskofu hao ambao walikuwa wanaongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Alinikisa Cheyo walimuomba Waziri Chikawe aingilie kati kwa kudhibiti vurugu hizo ambazo zinazisambaratisha kanisa lao. Hata hivyo, Waziri Chikawe aliahidi kulifanyia kazi suala hilo na atalitolea maamuzi baada ya kufanya uchunguzi wa kina kwa kukutana na pande zote mbili zinazogombana. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akimsikiliza kwa makini Askofu wa Kanisa la Moravian nchini, Conrad Nguvumali (watatu kulia) wakati wa mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi ya Waziri Chikawe jijini Dar es Salaam leo. Maaskofu watano wa Kanisa hilo ambalo limekumbwa na mgogoro kwa muda mrefu sasa, wakiongozwa na Askofu Kiongozi wa Kanisa hilo nchini, Alinikisa Cheyo (wapili kushoto) walionana na Waziri huyo ili kuomba msaada wake katika kudhibiti vurugu zinazoendelea katika Kanisa hilo. Hata hivyo, Waziri Chikawe aliahidi kulifanyia kazi na hatimaye kulitolea maamuzi suala hilo baada ya kufanya uchunguzi wa kina kwa kukutana na pande zote mbili zinazogombana. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment