Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akiwa ndani ya moja ya
nyumba za Wakimbizi waliopo katika Kituo cha Mpito cha Wakimbizi (NMC) kilichopo
mjini Kigoma. Katika nyumba hiyo Waziri Chikawe alizungumza na familia ya
mkimbizi kutoka nchini Kongo (kushoto) wanaoishi katika nyumba hiyo. Waziri Chikawe
yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi. Wapili kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika
la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole. Kituo
hicho kilichopo mjini humo kinawahifadhi wakimbizi zaidi ya 400 wakiwemo
wanaoenda kwenye matibabu, wanaoenda nchi ya tatu, wenye matatizo ya kiusalama,
na waomba hifadhi ya muda ya ukimbizi.
|
No comments:
Post a Comment