Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akizungumza na wajumbe wa Kamati ya
Ulinzi na Usalama katika kikao kilichoitishwa kwa ajili yake, na Mkuu wa Mkoa
wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu, Issa Machibya. Katika kikao hicho kilichofayika
katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi za Mkoa wa Kigoma, Waziri na Kamati hiyo
walijadiliana masuala mbalimbali ya Ulinzi na Usalama. Waziri Chikawe na
maafisa wake waliwasili mkoani humo leo kwa ajili ya ziara ya kikazi. Waziri
Chikawe licha ya kukutana na Kamati hiyo
ya mkoa, pia anatarajiwa kutembelea Kambi za Wakimbizi zilizopo mkoani humo.
|
No comments:
Post a Comment