Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kushoto) akizungumza
na wajumbe wa Baraza Dogo la Wafanyakazi la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kabla
ya kulizindua Baraza hilo katika Hoteli ya Livingstone mjini Bagamoyo leo. Katika
hotuba yake, Abdulwakil aliwataka viongozi wakuu wa jeshi hilo kushirikiana
kikamilifu na watumishi wote ili kuleta mabadiliko chanya ndani ya jeshi hilo.
Wapili kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Pius Nyambacha, Kulia ni
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi la
Zimamoto na Uokoaji, Shwaybu Mohamoud. Watatu kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Tume
ya Usuluhishi na Upatanishi (CMA), Andrew Mwalisisi na wapili kushoto ni Katibu
wa Tughe tawi hilo, Andason Kalewa.
|
No comments:
Post a Comment