WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Tuesday 23 June 2015

BANDA LA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI LAENDELEA KUNG'ARA KATIKA MAONYESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA

 Afisa Habari Mkuu  wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Rose Mdami (kulia) akitoa maelezo kwa mmoja wa wageni waliotembelea banda la Mamlaka hiyo kuhusu huduma zinazotolewa na Mamlaka hiyo, katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jjijini Dar es Salaam.

 Mwananchi aliyetembelea Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), akipewa maelezo na Afisa Habari Mkuu wa Mamlaka hiyo, Rose Mdami (kulia) kuhusu taarifa mbalimbali zinazoandaliwa na Mamlaka hiyo, katika maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja,jijini Dar es Salaam.


 Askari wa Jeshi la Polisi nchini,Tumaini Julius, akitoa maelezo kwa mwananchi aliyetembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi hilo,  katika maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jjijini Dar es Salaam.


 Mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akipiga picha  na  sanamu ya askari inayoonyesha mavazi yaliyokuwa yanavaliwa  na askari wa kike, katika maonesho hayo ya Wiki ya Utumishi wa Umma  yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja,jijini Dar es Salaam.

Mkaguzi Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji, Dickson Rweza (kushoto), akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma  yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. 

No comments:

Post a Comment