WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Tuesday 29 September 2015

WAKIMBIZI KUTOKA BURUNDI WAENDELEA KUWASILI KATIKA KAMBI YA NYARUGUSU ILIYOKO WILAYANI KASULU MKOANI KIGOMA

Mkimbizi  kutoka  Burundi,  Philipo Nyandungulu,   akishuka  kutoka  kwenye  basi  baada  ya  kuwasili katika  kambi  ya  wakimbizi  ya  Nyarugusu  iliyoko  Kasulu  mkoani  Kigoma.   Idadi  ya  wakimbizi  kutoka  Burundi  imekuwa  ikiongezeka  siku  hadi  siku  na  Wizara  ya  Mambo  ya Ndani ya Nchi kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi (UNHRC) imekuwa ikiwahifadhi kwa muda katika kambi hiyo.
Baadhi ya wakimbizi kutoka nchini Burundi, wanaohifadhiwa katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma, wakiwapokea wakimbizi wenzao (hawapo pichani) waliowasili jana kwa basi kwa ajili ya kuhifadhiwa katika kambi hiyo.
Mkimbizi kutoka Burundi,Philipo Nyandugulu(kushoto)   na mkewe Vanisi Nyandugulu,  wakisubiri taratibu za kupangiwa sehemu ya kuishi baada ya kuwasili katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma, baada ya kuwasili katika kambi hiyo jana.
Mkimbizi kutoka Burundi, Vanisi Nyandugulu akipanga vifaa vyake baada ya kuwasili katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma jana.  Wakimbizi kutoka Burundi wanaendela kuwasili nchini ambapo wanahifadhiwa katika kambi ya wakimizi ya Nyarugusu.
Koplo Flora Peter  wa Kituo cha Polisi katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu akiwa ameshikilia visu, panga na fimbo vilivyokutwa katika baadhi ya mizigo ya wakimbizi kutoka Burundi wanaowasili katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma.  Vifaa vya hatari kama vile visu, panga, fimbo na mishale haviruhusiwi kumilikiwa na wakimbizi wapya wanaowasili kambini hapo, kwa sababu za kiusalama.
Mkimbizi kutoka Burundi,  Nibaruja Europernce , akihamasisha wenzake wanaowasili katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma kuhusu taratibu za kuishi kambini hapo ikiwani ni pamoja na kutekeleza masuala muhimu ya kiafya, jana.
Mfanyakazi wa Shirika la Maji na Usafi wa Mazingira (TWESA) linalofanya shughuli zake katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma, Andrea Niyitanga , Akimnawisha mikono kwa kutumia maji yaliyowekwa dawa, mkimbizi kutoka Burundi ikiwa ni mojawapo ya mkakati wa kutoa elimu ya afya.
Mtoto Olivia Nekwizera, ambaye ni mkimbizi kutoka Burundi akisaidiwa na mama yake kunawa mikono baada ya kuwasili katika kambi ya wakimizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Kunawa mikono kwa maji yenye dawa ni jambo la lazima kwa wakimbizi wapya kuonyesha umuhimu wa kuzingatia masuala ya afya na pia kudhibiti magonjwa ya kuambukiza.
Watoto wa moja ya familia ya wakimbizi kutoka Burundi wakielekezwa kuingia katika makazi yao mara baada ya kuwasili katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko katika wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma. Anayeelekeza ni mfanyakazi wa Shirika la Maji na Usafi wa Mazingira (TWESA) linalofanya shughuli zake katika kambi hiyo.
Wakimbizi kutoka Burundi wakipata maelezo ya jinsi ya kuishi katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma mara baada ya kuwasili kambini hapo.  Anayetoa maelekezo hayo ni Nayiga Mireye wa Shirika la Maji na Usafi wa Mazingira (TWESA) linalofanya shughuli zake kambini hapo.


No comments:

Post a Comment