Mkuu
wa Kambi ya Wakimbizi ya Nduta, wilayani Kibondo, Fred Nsijile akitoa taarifa
ya kambi yake kwa Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa (kushoto). Katika
taarifa hiyo Mkuu wa Kambi alisema kambi yake inakabiliwa na upungufu wa maji
kutokana na idadi kubwa ya wakimbizi wanaoishi kambini humo. Hata hivyo katika
hotuba yake, Waziri Mkuu Majaliwa alisema atalifanyia kazi tatizo hilo na pia aliwaonya
wakimbizi katika kambi hiyo kutojihusisha na uhalifu ili waweze kuishi kwa
usalama katika eneo waliohifadhiwa. Wapili kushoto meza kuu ni Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga. Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la
Kujenga Taifa, Job Masima (watatu kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi,
Harrison Mseke.
|
No comments:
Post a Comment