WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Saturday 30 January 2016

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI ATEMBELEA MRADI WA UMWAGILIAJI GEREZA LA KILIMO IDETE, MKOANI MOROGORO

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, Mhe. Balozi Simba Yahya akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Magereza mara baada ya kuwasili gerezani hapo kwa ziara ya kikazi Januari 29, 2016 kujionea ujenzi wa mradi wa umwagiliaji Gereza la Kilimo Idete lililopo Wilaya ya Kilombero, Mkoani Morogoro(anayefuatia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Balozi Simba Yahya(wa pili kulia) akiwa ameongozana na Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa kwanza kushoto) kuelekea katika Ukumbi wa Gereza hilo kwa ajili ya kupata taarifa kamili ya utekelezaji wa mradi wa umwagiliaji Gereza la Kilimo Idete kutoka kwa Wakandarasi wa mradi na Mshauri Mwelekezi mradi(kulia) ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombero, Bw. Yahya Sinaniya.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Balozi Simba Yahya akiangalia sehemu ya banio la kutunzia maji ya mradi wa Gereza la Kilimo Idete akiwa pamoja na msafara wa Wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi(wa kwanza kushoto) ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Manunuzi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Manyama Mapesi(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Muonekano wa mfereji wa maji yatakayokuwa yakitumika katika mradi wa umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Mkoani Morogoro kama inavyoonekana katika picha.

Mshauri wa Mradi, Mhandisi Nzobonaliba Imani akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Balozi Simba Yahya(katikati) alipotembelea mradi wa umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete lililopo Mkoani Morogoro(kulia) ni Mkuu wa Gereza hilo, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Nsajigwa Mwakenja wakiaangalia ujenzi wa mradi wa umwagiliaji wa Gereza hilo.
Wakandarasi wa Kampuni ya ujenzi wa mradi wa umwagiliaji wa Gereza Kilimo Idete, lililopo Mkoani Morogoro wakiendelea na ujenzi wa mifereji ya maji kama inavyoonekana katika picha.

Wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakipata maelezo ya Kitaalam kutoka kwa Mshauri Mwelekezi walipotembelea mradi huo kujionea hatua mbalimbali za ujenzi. Wengine ni Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya ya Kilombero.

No comments:

Post a Comment