Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akizungumza na Makamanda wa Jeshi
la Zimamoto na Uokoaji wakiongozwa na
Kamishna Jenerali, Pius Nyambacha (kulia kwa Waziri) wakati Waziri huyo
alipofanya ziara Makao Makuu ya Jeshi hilo, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es
Salaam leo. Katika ziara hiyo, Waziri Kitwanga aliliagiza Jeshi hilo
kumchukulia hatua kali za kisheria kwa yeyote atakaye kiuka kulipisha gari la
Zimamoto na Uokoaji wakati linaenda katika tukio lolote la uokoaji pamoja na
kuzima moto. Pia aliitaka Jeshi hilo kuongeza kasi ya kukusanya mapato katika
vyanzo vyake mbalimbali.
|
Mkufunzi
wa Masuala ya Majanga wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Christopher Marwa
(kulia) akimuonyesha Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga
(aliyevaa tai), gari la Uokozi ambalo lina vifaa mbalimbali vya uokozi. Waziri
Kitwanga alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi hilo, na baadaye
kujifunza kazi mbalimbali za jeshi hilo katika Kituo cha Zimamoto Kanda ya
Ilala, jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake, Waziri Kitwanga aliliagiza
Jeshi hilo kumchukulia hatua kali za kisheria kwa yeyote atakaye kiuka
kulipisha gari la Zimamoto na Uokoaji wakati linaenda katika tukio lolote la
uokoaji pamoja na kuzima moto. Pia aliitaka Jeshi hilo kuongeza kasi ya
kukusanya mapato katika vyanzo vyake mbalimbali. Picha na Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi.
|
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akizungumza waandishi wa habari
mara baada ya kumaliza ziara yake katika Kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake kwa waandishi hao wa
habari, Waziri Kitwanga aliliagiza Jeshi hilo kumchukulia hatua kali za
kisheria kwa mtu yeyote atakaye kiuka kulipisha gari la Zimamoto na Uokoaji
wakati linaenda katika tukio lolote la uokoaji pamoja na kuzima moto. Pia
aliitaka Jeshi hilo kuongeza kasi ya kukusanya mapato katika vyanzo vyake
mbalimbali.
|
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akiondoka Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mara baada ya kuzungumza na Makamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakiongozwa na Kamishna Jenerali, Pius Nyambacha (kulia). Katika hotuba yake kwa viongozi hao wa jeshi, Waziri Kitwanga aliliagiza Jeshi hilo kumchukulia hatua kali za kisheria kwa yeyote atakaye kiuka kulipisha gari la Zimamoto na Uokoaji wakati linaenda katika tukio lolote la uokoaji pamoja na kuzima moto. Pia aliitaka Jeshi hilo kuongeza kasi ya kukusanya mapato katika vyanzo vyake mbalimbali. |
No comments:
Post a Comment